Tuesday, October 2, 2012

JUMA NATURE KUACHIA NGOMA NA BABY MADAHA

Juma Nature, Baby Madaha, Mike Tee katika mchakato wa kutayarisha video mpya ya Kibra na Baby Madaha
Imekuwa safari ndefu katika muziki wa Hip Hop kwa Juma Nature kama kiongozi wa kundi mahiri la Hip Hop, Wanaume Halisi. Akiwa na zaidi ya miaka 10 kwenye 'gemu', Juma Nature aka Kibra ni kama veteran katika gemu lakini bado ana 'njaa' ya muziki kama mwanamuziki anayechipukia.

Kwa muda mrefu Wanaume Halisi wamekuwa kimya na hii inatokana na sababu kwamba wamekuwa wakitayarisha nyimbo kwa ajili ya ujio mpya. Na kwa kuthibitisha kwamba huu ni ujio mpya, walimsaini Baby Madaha kama member mpya wa kundi lao na wamefanya ngoma moja matata ambayo itaachiwa  hewani pindi video yake, ambayo inatengenezwa na Mike Tee, itakapokuwa tayari.



Akiongelea hiyo ngoma Juma Nature alikuwa na haya ya kusema "Watu wengine wanatoka kijijini na kuja mjini wakijua kwamba itakuwa fresh, ila wakishafika mjini mambo yanakuwa ndivyo sivyo, that's why ukaona tumefanya ngoma kama hii. Hii ngoma inamuonyesha mtu aliyetoka kijijini ambako alikuwa fresh tu na mali za kutosha ila akashawishika kuja mjini ambako mchezo ukawa mgumu kwake mwishowe akaharibu, kumbe town kuwa watu wake , wenye mji wao. Baadaye akagundua kumbe Bongo huku cheche, hakumfai, akaamua kurudi zake kijijini alipokuzoea."

hii ni katika harakati za utayarishwaji wa video mpaya ya Juma Nature na Baby Madaha

Katika kutia vionjo ujio wao mpya, Wanaume Halisi walimsaini Baby Madaha ambaye ni zao la shoo maarufu ya Bongo Star Search. Anajulikana zaidi kwa ngoma kali kama Amore na Desperado ambazo zote zimefanikiwa kumuweka juu katika tasnia ya muziki wa Bongo, lakini zaidi anajulikana kwa vituko vyake vya hapa na pale ambavyo vinafanya jina lake kuwa habari ya mujini.

Baby Madaha katika pozi
Mbali na yote hayo, uwepo wa Baby Madaha ndani ya kundi la Wanaume halisi ni sababu tosha ya kulifanya kundi hilo kuwa mojawapo ya makundi bora zaidi katika kiwanda cha muziki wa Bongo. Mchanganyiko wa sauti nzuri ya Baby Madaha na sauti ya Nature au Dollo au hata KR, ni mwanzo wa changamoto kubwa sana kwa makundi mengine ya muziki wa Hip Hop hapa Bongo na hata nje ya mipaka yetu katika kuboresha mwenendo mzima wa muziki wa kizazi kipya.


Kaa tayari kwa ujio mpya, Kaa tayari kwa ngoma mpya ya Juma Nature na Baby Madaha.

No comments:

Post a Comment